11 Kesho yake, baada ya Pasaka, siku hiyohiyo wakaanza kula mazao ya nchi, yaani, mikate isiyo na chachu+ na nafaka zilizokaangwa. 12 Mana ilikoma siku iliyofuata, baada ya Waisraeli kula baadhi ya mazao ya nchi; Waisraeli hawakupata mana tena,+ wakaanza kula mazao ya nchi ya Kanaani mwaka huo.+