-
Yoshua 8:30, 31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Kisha Yoshua akamjengea Yehova Mungu wa Israeli madhabahu kwenye Mlima Ebali,+ 31 kama Musa mtumishi wa Yehova alivyowaamuru Waisraeli na kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Sheria+ ya Musa: “Madhabahu ya mawe ambayo hayakuchongwa wala kuguswa na kifaa chochote cha chuma.”+ Na juu yake wakamtolea Yehova dhabihu za kuteketezwa na pia dhabihu za ushirika.+
-