-
Mambo ya Walawi 6:2-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 “Mtu akitenda dhambi na kukosa uaminifu kwa Yehova+ kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa atunze,+ au alichoachiwa kama dhamana, au akimwibia au kumlaghai jirani yake, 3 au akipata kitu kilichopotea na kudanganya kwamba hajakipata, naye akiapa kwa uwongo kuhusu dhambi yoyote kama hiyo ambayo huenda akatenda,+ anapaswa kufanya hivi: 4 Ikiwa ametenda dhambi naye ana hatia, ni lazima arudishe kitu alichoiba, kitu alichochukua kwa nguvu, kitu alichochukua kwa ulaghai, kitu alichokabidhiwa atunze, au kitu kilichopotea akakipata, 5 au chochote alichoapia kwa uwongo, ni lazima alipe kitu hicho kikamili+ na kuongeza sehemu ya tano ya thamani yake. Atamrudishia mwenyewe kitu hicho siku ambayo hatia yake itajulikana.
-