21 Ifuatayo ni orodha ya vitu vilivyotumiwa kutengeneza hema la ibada, yaani, hema la Ushahidi.+ Orodha hii ilitayarishwa kwa amri ya Musa, na lilikuwa jukumu la Walawi+ kuitayarisha chini ya uongozi wa Ithamari+ mwana wa Haruni kuhani.
16 Musa akamtafuta sana mbuzi wa dhabihu ya dhambi,+ lakini akagundua kwamba alikuwa ameteketezwa. Kwa hiyo akawakasirikia sana Eleazari na Ithamari, wana waliobaki wa Haruni, akawauliza:
2 Hata hivyo, Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao,+ nao hawakuwa na wana wowote; lakini Eleazari+ na Ithamari waliendelea kutumikia wakiwa makuhani.