Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 29:10-14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Sasa utamleta yule ng’ombe dume mbele ya hema la mkutano, na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ng’ombe dume.+ 11 Mchinje huyo ng’ombe dume mbele za Yehova, kwenye mlango wa hema la mkutano.+ 12 Chukua kiasi fulani cha damu ya huyo ng’ombe dume kwa kidole chako na kuitia kwenye pembe za madhabahu,+ kisha umwage damu yote inayobaki chini kwenye msingi wa madhabahu.+ 13 Kisha chukua mafuta yote+ yanayofunika matumbo, mafuta yaliyo juu ya ini, na figo zake mbili na mafuta yaliyo juu yake, nawe uchome moto vitu hivyo ili vifuke moshi juu ya madhabahu.+ 14 Lakini nyama ya ng’ombe dume huyo na ngozi yake na mavi yake utaviteketeza nje ya kambi. Hiyo ni dhabihu ya dhambi.

  • Mambo ya Walawi 4:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 “‘Kuhani aliyetiwa mafuta+ akitenda dhambi+ na kuwaletea watu hatia, basi atamtolea Yehova ng’ombe dume mchanga asiye na kasoro, kuwa dhabihu ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda.+ 4 Atamleta huyo ng’ombe dume kwenye mlango wa hema la mkutano+ mbele za Yehova na kuweka mkono wake juu ya kichwa cha ng’ombe dume huyo, naye atamchinja mbele za Yehova.+

  • Mambo ya Walawi 16:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 “Kisha Haruni atamtoa yule ng’ombe dume wa dhabihu ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe, naye atatoa dhabihu ya kufunika dhambi zake mwenyewe+ na za nyumba yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki