- 
	                        
            
            2 Mambo ya Nyakati 17:8, 9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
8 Walikuwa pamoja na Walawi wafuatao: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobaya, na Tob-adoniya, pamoja na kuhani Elishama na kuhani Yehoramu.+ 9 Walianza kufundisha nchini Yuda, wakiwa na kitabu cha Sheria ya Yehova,+ nao walizunguka katika majiji yote ya Yuda wakiwafundisha watu.
 
 - 
                                        
 
- 
	                        
            
            Nehemia 8:7, 8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
7 Nao Yeshua, Bani, Sherebia,+ Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi,+ Hanani, na Pelaya, waliokuwa Walawi, walikuwa wakiwafafanulia watu Sheria,+ huku watu wakiwa wamesimama. 8 Wakaendelea kukisoma kitabu hicho kwa sauti kubwa, wakaisoma Sheria ya Mungu wa kweli, huku wakiifafanua waziwazi na kueleza maana yake; hivyo wakawasaidia watu kuelewa mambo yaliyokuwa yakisomwa.*+
 
 -