Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 33:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Acha wamfundishe Yakobo amri zako*+

      Na Waisraeli Sheria yako.+

      Acha wakufukizie uvumba wenye harufu inayokupendeza*+

      Na dhabihu nzima ya kuteketezwa kwenye madhabahu yako.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 17:8, 9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Walikuwa pamoja na Walawi wafuatao: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobaya, na Tob-adoniya, pamoja na kuhani Elishama na kuhani Yehoramu.+ 9 Walianza kufundisha nchini Yuda, wakiwa na kitabu cha Sheria ya Yehova,+ nao walizunguka katika majiji yote ya Yuda wakiwafundisha watu.

  • Nehemia 8:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Nao Yeshua, Bani, Sherebia,+ Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi,+ Hanani, na Pelaya, waliokuwa Walawi, walikuwa wakiwafafanulia watu Sheria,+ huku watu wakiwa wamesimama. 8 Wakaendelea kukisoma kitabu hicho kwa sauti kubwa, wakaisoma Sheria ya Mungu wa kweli, huku wakiifafanua waziwazi na kueleza maana yake; hivyo wakawasaidia watu kuelewa mambo yaliyokuwa yakisomwa.*+

  • Malaki 2:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwa maana midomo ya kuhani inapaswa kulinda ujuzi, na watu wanapaswa kutafuta sheria* kutoka kinywani mwake,+ kwa sababu yeye ni mjumbe wa Yehova wa majeshi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki