-
Nehemia 8:7, 8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Nao Yeshua, Bani, Sherebia,+ Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi,+ Hanani, na Pelaya, waliokuwa Walawi, walikuwa wakiwafafanulia watu Sheria,+ huku watu wakiwa wamesimama. 8 Wakaendelea kukisoma kitabu hicho kwa sauti kubwa, wakaisoma Sheria ya Mungu wa kweli, huku wakiifafanua waziwazi na kueleza maana yake; hivyo wakawasaidia watu kuelewa mambo yaliyokuwa yakisomwa.*+
-
-
Ezekieli 44:23, 24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 “‘Wanapaswa kuwafundisha watu wangu tofauti kati ya kitu kitakatifu na kitu cha kawaida; nao watawafundisha tofauti kati ya kitu kisicho safi na kitu kilicho safi.+ 24 Wanapaswa kuwa waamuzi katika kesi;+ ni lazima wahukumu kulingana na sheria zangu.*+ Wanapaswa kufuata sheria zangu na amri zangu zinazohusu sherehe zangu zote+ na kuzitakasa sabato zangu.
-