Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 24:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 “Ikiwa ugonjwa wa ukoma* umetokea na kuenea, muwe waangalifu sana kufanya mambo yote ambayo makuhani Walawi watawaagiza mfanye.+ Muwe waangalifu kufanya kama tu nilivyowaamuru.

  • 2 Mambo ya Nyakati 15:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kwa muda mrefu* Waisraeli hawakuwa na Mungu wa kweli, hawakuwa na kuhani wa kuwafundisha, na hawakuwa na sheria.+

  • Nehemia 8:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Nao Yeshua, Bani, Sherebia,+ Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi,+ Hanani, na Pelaya, waliokuwa Walawi, walikuwa wakiwafafanulia watu Sheria,+ huku watu wakiwa wamesimama. 8 Wakaendelea kukisoma kitabu hicho kwa sauti kubwa, wakaisoma Sheria ya Mungu wa kweli, huku wakiifafanua waziwazi na kueleza maana yake; hivyo wakawasaidia watu kuelewa mambo yaliyokuwa yakisomwa.*+

  • Ezekieli 44:23, 24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 “‘Wanapaswa kuwafundisha watu wangu tofauti kati ya kitu kitakatifu na kitu cha kawaida; nao watawafundisha tofauti kati ya kitu kisicho safi na kitu kilicho safi.+ 24 Wanapaswa kuwa waamuzi katika kesi;+ ni lazima wahukumu kulingana na sheria zangu.*+ Wanapaswa kufuata sheria zangu na amri zangu zinazohusu sherehe zangu zote+ na kuzitakasa sabato zangu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki