-
Mambo ya Walawi 5:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 “Mtu akikosa uaminifu kwa kutenda dhambi bila kukusudia kwa kuvunja sheria kuhusu vitu vitakatifu vya Yehova,+ anapaswa kumletea Yehova kondoo dume asiye na kasoro kutoka kundini ili awe dhabihu ya hatia;+ thamani yake itapimwa kwa shekeli za fedha* kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.*+ 16 Naye atalipia dhambi aliyotenda dhidi ya mahali patakatifu na pia ataongeza sehemu ya tano ya thamani ya vitu hivyo.+ Atampa kuhani, ili kuhani amtolee dhabihu ya kufunika dhambi+ yake akitumia kondoo dume wa dhabihu ya hatia, naye atasamehewa.+
-