- 
	                        
            
            Luka 6:34, 35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
34 Pia, mkiwakopesha* wale tu ambao mnatumaini watawalipa, mnapata faida gani?+ Hata watenda dhambi huwakopesha watenda dhambi ili warudishiwe kiasi kilekile. 35 Badala yake, endeleeni kuwapenda adui zenu, kutenda mema, na kukopesha bila kutumaini kurudishiwa;+ nanyi mtapata thawabu kubwa, na mtakuwa wana wa Aliye Juu Zaidi, kwa sababu yeye huwaonyesha fadhili hata watu wasio na shukrani na waovu.+
 
 -