-
Mambo ya Walawi 25:35, 36Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
35 “‘Ikiwa ndugu yako aliye karibu nawe amekuwa maskini na hawezi kujiruzuku, unapaswa kumsaidia,+ kama ambavyo ungemsaidia mgeni na pia mhamiaji,+ ili aendelee kuwa hai kama wewe. 36 Usimtoze riba au kujipatia faida kutoka kwake.+ Ni lazima umwogope Mungu wako,+ na ndugu yako ataendelea kuwa hai kama wewe.
-
-
Kumbukumbu la Torati 15:7, 8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 “Ikiwa mmoja wa ndugu zenu atakuwa maskini miongoni mwenu katika mojawapo ya majiji yaliyo katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, msiifanye mioyo yenu iwe migumu au kumfumbia mkono ndugu yenu maskini.+ 8 Kwa maana mnapaswa kumfumbulia mkono wenu kwa ukarimu+ na kufanya yote mwezayo kumkopesha* chochote anachohitaji au alichopungukiwa.
-