Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 15:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “Ikiwa mmoja wa ndugu zenu atakuwa maskini miongoni mwenu katika mojawapo ya majiji yaliyo katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, msiifanye mioyo yenu iwe migumu au kumfumbia mkono ndugu yenu maskini.+

  • Zaburi 41:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 41 Mwenye furaha ni mtu yeyote anayemjali mtu wa hali ya chini;+

      Yehova atamwokoa siku ya msiba.

  • Zaburi 112:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Mambo humwendea vema mtu anayekopesha kwa ukarimu.*+

      י [Yod]

      Hufanya mambo yake kwa haki.

  • Methali 3:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Usiwanyime mema wale unaopaswa kuwatendea mema*+

      Ikiwa una uwezo wa kuwasaidia.*+

  • Methali 19:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova,+

      Naye Atamlipa* kwa anayotenda.+

  • Marko 14:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwa maana maskini mnao sikuzote,+ na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka, lakini mimi hamtakuwa nami sikuzote.+

  • Matendo 11:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Basi wanafunzi wakaamua kila mmoja kulingana na uwezo wake,+ watume msaada*+ kwa akina ndugu walioishi Yudea;

  • 1 Timotheo 6:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Waambie watende mema, wawe matajiri katika matendo mazuri, wawe wakarimu, tayari kushiriki vitu na wengine,+

  • 1 Yohana 3:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Lakini yeyote aliye na mali za ulimwengu huu akimwona ndugu yake akiwa na uhitaji naye akatae kumhurumia, anawezaje kuwa na upendo wa Mungu ndani yake?+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki