7 Halafu akachukua kitabu cha agano na kuwasomea watu kwa sauti.+ Nao wakasema: “Mambo yote ambayo Yehova amesema tuko tayari kuyafanya, nasi tutatii.”+
16 Sasa Yehova akamwambia Musa hivi: “Tazama! Unakaribia kufa,* na watu hawa wataanza kufanya ukahaba wa kiroho pamoja na miungu ya kigeni inayowazunguka katika nchi wanayoenda.+ Wataniacha na kuvunja agano langu+ ambalo nimefanya pamoja nao.+
9 Halitakuwa kama agano nililofanya pamoja na mababu zao siku niliyowashika mkono na kuwaongoza kutoka nchini Misri,+ kwa sababu hawakuendelea kulishika agano langu, basi nikaacha kuwajali,’ asema Yehova.*