-
Mambo ya Walawi 23:27-31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
27 “Hata hivyo, siku ya kumi ya mwezi huo wa saba ni Siku ya Kufunika Dhambi.+ Mtakuwa na kusanyiko takatifu, nanyi mnapaswa kujitesa*+ na kumtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. 28 Hampaswi kufanya kazi yoyote siku hiyo kwa sababu ni siku ya kufunika dhambi+ zenu mbele za Yehova Mungu wenu. 29 Mtu yeyote ambaye hatajitesa* siku hiyo atauawa.+ 30 Nami nitamwangamiza mtu yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo. 31 Hampaswi kufanya kazi yoyote. Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote mahali popote mtakapoishi.
-