-
Waebrania 9:24-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Kwa maana Kristo hakuingia mahali patakatifu palipotengenezwa kwa mikono,+ ambapo ni mfano wa uhalisi,+ bali aliingia mbinguni kwenyewe,+ hivi kwamba sasa anaonekana mbele za* Mungu kwa ajili yetu.+ 25 Hilo halikufanywa ili ajitoe mwenyewe mara nyingi, kama kuhani mkuu anavyoingia mahali patakatifu mwaka baada ya mwaka+ akiwa na damu ambayo si yake mwenyewe. 26 La sivyo, ingekuwa lazima ateseke mara nyingi tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu. Lakini sasa amejifunua mara moja kwa wakati wote kwenye umalizio wa mifumo ya mambo* ili kuondoa dhambi kupitia dhabihu yake mwenyewe.+
-