-
Hesabu 28:3-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 “Nawe uwaambie, ‘Hii ndiyo dhabihu inayochomwa kwa moto ambayo mtamtolea Yehova: mtatoa kwa ukawaida kila siku wanakondoo dume wawili wasio na kasoro wenye umri wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa.+ 4 Mtamtoa mwanakondoo dume mmoja asubuhi, na mwanakondoo dume wa pili mtamtoa jioni kabla ya giza kuingia,*+ 5 pamoja na toleo la nafaka la sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja* ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini* ya mafuta ya zeituni zilizopondwa.+ 6 Ni dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida,+ iliyoanzishwa kwenye Mlima Sinai, dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova, 7 pamoja na toleo lake la kinywaji la robo ya hini kwa ajili ya kila mwanakondoo dume.+ Mimineni kileo mahali patakatifu kikiwa toleo la kinywaji mbele za Yehova. 8 Nanyi mtamtoa mwanakondoo dume wa pili jioni kabla ya giza kuingia.* Mtamtoa pamoja na toleo la nafaka kama lile lililotolewa asubuhi pamoja na toleo lake la kinywaji. Mtamtoa akiwa dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.+
-