53 Walawi wanapaswa kupiga kambi kuzunguka hema la Ushahidi, ili hasira yangu isiwawakie Waisraeli;+ na lazima Walawi wawajibike kulitunza* hema la Ushahidi.”+
19 Lakini Mungu akawaua watu wa Beth-shemeshi, kwa sababu walilitazama Sanduku la Yehova. Aliwaua watu 50,070* miongoni mwao, basi watu wakaanza kuomboleza kwa sababu Yehova alikuwa amewaua kwa mauaji makubwa.+