-
Hesabu 4:15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 “Ni lazima Haruni na wanawe wamalize kufunika mahali patakatifu+ na vyombo vyote vya mahali patakatifu kabla ya watu kuanza safari. Kisha wana wa Kohathi watakuja kuvibeba,+ lakini hawapaswi kugusa vitu vitakatifu, la sivyo watakufa.+ Wana wa Kohathi ndio walio na jukumu la kubeba vitu vya hema la mkutano.
-
-
Hesabu 4:24-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Huu ndio utumishi ambao watu wa familia za Wagershoni wamegawiwa kufanya na vitu wanavyopaswa kubeba:+ 25 Watabeba vitambaa vya hema la ibada,+ hema la mkutano, kifuniko chake na kifuniko cha ngozi ya sili kilicho juu yake,+ pazia la mlango wa hema la mkutano,+ 26 mapazia ya ua yanayoning’inia,+ pazia la mlango wa ua+ unaozunguka hema la ibada na madhabahu, kamba za hema hilo na vyombo vyake vyote, na vitu vyote vinavyotumiwa katika utumishi wa hema la ibada. Hiyo ndiyo kazi waliyogawiwa.
-
-
Hesabu 4:31-33Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Ni jukumu lao kubeba+ vitu vifuatavyo vinavyohusiana na utumishi wao katika hema la mkutano: viunzi+ vya hema la ibada, fito zake,+ nguzo zake,+ vikalio vyake;+ 32 nguzo+ za ua unaozunguka pande zote, vikalio vyake,+ vigingi vyake vya hema,+ na kamba za hema hilo pamoja na vifaa vyake vyote na utumishi wote unaohusiana na hema la ibada. Utamgawia kila mmoja wao kwa jina vifaa anavyopaswa kubeba. 33 Hivyo ndivyo familia za wana wa Merari+ zitakavyotumikia katika hema la mkutano chini ya usimamizi wa Ithamari mwana wa kuhani Haruni.”+
-