-
Hesabu 10:11-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Basi katika mwaka wa pili, mwezi wa pili, siku ya 20 ya mwezi huo,+ lile wingu liliinuka kutoka juu ya hema+ la Ushahidi. 12 Kwa hiyo Waisraeli wakaanza kuondoka katika nyika ya Sinai kulingana na utaratibu uliowekwa wa kuondoka,+ na wingu hilo likasimama katika nyika ya Parani.+ 13 Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwao kuondoka kama Yehova alivyokuwa amewaagiza kupitia Musa.+
-