Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Mambo ya Nyakati 15:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Waisraeli wote walikuwa wakilipandisha sanduku la agano la Yehova kwa kelele za shangwe,+ wakipiga pembe, tarumbeta,+ matoazi, na kupiga kwa sauti kubwa vinanda na vinubi.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 5:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 waimbaji wote Walawi+ walioongozwa na Asafu,+ Hemani,+ Yeduthuni,+ wana wao na ndugu zao walikuwa wamevaa mavazi ya kitambaa bora, wakiwa wamebeba matoazi, vinanda, na vinubi; walikuwa wamesimama upande wa mashariki wa madhabahu, na makuhani 120 waliokuwa wakipiga tarumbeta walikuwa pamoja nao.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 7:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Makuhani walikuwa wamesimama katika vituo vyao vya kazi, na Walawi pia waliokuwa na ala za muziki zilizopigwa kuambatana na nyimbo ambazo Yehova aliimbiwa.+ (Mfalme Daudi alikuwa ametengeneza ala hizo ili kumshukuru Yehova—“kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele”—wakati Daudi alipokuwa akitoa sifa pamoja nao.*) Na makuhani walikuwa wakipiga tarumbeta kwa sauti kubwa+ mbele yao, huku Waisraeli wote wakiwa wamesimama.

  • Ezra 3:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Wajenzi walipoweka msingi wa hekalu la Yehova,+ makuhani waliovaa mavazi rasmi, wakiwa na tarumbeta,+ na Walawi, wana wa Asafu, wakiwa na matoazi, wakasimama ili kumsifu Yehova kulingana na maagizo ya Mfalme Daudi wa Israeli.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki