3 na kuwaamuru watu, “Mara tu mtakapoliona sanduku la agano la Yehova Mungu wenu likiwa limebebwa na makuhani Walawi,+ mwondoke na kulifuata, 4 ili mjue njia ya kupita kwa kuwa hamjawahi kupita njia hiyo, lakini muwe umbali wa mikono 2,000 hivi kutoka kwenye sanduku hilo; msilikaribie zaidi.”