8 Nitashuka huko ili niwaokoe kutoka mikononi mwa Wamisri+ na kuwapandisha kutoka katika nchi hiyo na kuwapeleka katika nchi nzuri na kubwa, nchi inayotiririka maziwa na asali,+ eneo la Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.+
24 Ndiyo sababu niliwaambia: “Mtaimiliki nchi yao, nami nitawapa iwe miliki yenu, nchi inayotiririka maziwa na asali.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu, nami nimewatenga na mataifa mengine.”+