-
Mambo ya Walawi 21:10-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 “‘Kuhani mkuu miongoni mwa ndugu zake, aliyetiwa mafuta kichwani+ na kuwekwa rasmi ili avae mavazi ya kuhani,+ anapaswa kutunza nywele zake na hapaswi kurarua mavazi yake.+ 11 Hapaswi kumkaribia mtu yeyote aliyekufa;*+ hapaswi hata kujichafua kwa kumgusa baba yake au mama yake ambaye amekufa. 12 Hapaswi kuondoka mahali patakatifu wala kuchafua mahali patakatifu pa Mungu wake,+ kwa sababu ishara ya wakfu, yale mafuta ya Mungu wake yanayotumiwa kutia mafuta+ yako juu yake. Mimi ni Yehova.
-