-
Hesabu 16:39, 40Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
39 Basi kuhani Eleazari akachukua vyetezo vya shaba vilivyoletwa na wale wanaume waliokuwa wameteketezwa, akavipiga na kuvinyoosha ili vifunike madhabahu, 40 kama Yehova alivyomwambia kupitia Musa. Viliwakumbusha Waisraeli kwamba mtu yeyote asiye na idhini* ambaye si mzao wa Haruni hapaswi kukaribia madhabahu ili kumfukizia Yehova+ uvumba na kwamba mtu yeyote asiwe kama Kora na wale waliomuunga mkono.+
-