Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 16:39, 40
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 Basi kuhani Eleazari akachukua vyetezo vya shaba vilivyoletwa na wale wanaume waliokuwa wameteketezwa, akavipiga na kuvinyoosha ili vifunike madhabahu, 40 kama Yehova alivyomwambia kupitia Musa. Viliwakumbusha Waisraeli kwamba mtu yeyote asiye na idhini* ambaye si mzao wa Haruni hapaswi kukaribia madhabahu ili kumfukizia Yehova+ uvumba na kwamba mtu yeyote asiwe kama Kora na wale waliomuunga mkono.+

  • 1 Samweli 6:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Lakini Mungu akawaua watu wa Beth-shemeshi, kwa sababu walilitazama Sanduku la Yehova. Aliwaua watu 50,070* miongoni mwao, basi watu wakaanza kuomboleza kwa sababu Yehova alikuwa amewaua kwa mauaji makubwa.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 26:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Hata hivyo, mara tu alipokuwa na nguvu, moyo wake ukawa na kiburi ambacho kilisababisha aangamie, naye alikosa kutenda kwa uaminifu kumwelekea Yehova Mungu wake kwa kuwa aliingia katika hekalu la Yehova ili kufukiza uvumba kwenye madhabahu ya uvumba.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 26:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Wakamkabili Mfalme Uzia na kumwambia: “Si vyema kwako, Uzia, kumfukizia Yehova uvumba!+ Ni makuhani tu wanaopaswa kufukiza uvumba, kwa maana wao ni wazao wa Haruni,+ waliotakaswa. Toka mahali patakatifu, kwa maana hujatenda kwa uaminifu, na kwa sababu hiyo hutapokea utukufu wowote kutoka kwa Yehova Mungu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki