12 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Panda uje kwangu mlimani na ukae huku. Nitakupa mabamba ya mawe yenye sheria na amri nitakazoandika ili kuwafundisha watu.”+
18 Sasa mara tu alipomaliza kuzungumza naye kwenye Mlima Sinai, alimpa Musa mabamba mawili ya Ushahidi,+ mabamba ya mawe yaliyoandikwa kwa kidole cha Mungu.+
19 Mara tu Musa alipoikaribia kambi na kuona ile sanamu ya ndama+ na watu wakicheza dansi, akaanza kuwaka hasira, naye akayatupa chini yale mabamba mawili yaliyokuwa mikononi mwake, yakavunjika-vunjika chini ya mlima.+
34Kisha Yehova akamwambia Musa: “Jichongee mabamba mawili ya mawe kama yale ya kwanza,+ nami nitaandika kwenye mabamba hayo maneno yaliyokuwa kwenye yale mabamba ya kwanza+ uliyoyavunja.+