-
Hesabu 13:23-27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Walipofika kwenye Bonde la Eshkoli,+ walikata tawi lenye kishada kimoja cha zabibu, na wanaume wawili wakalibeba kwa ufito pamoja na makomamanga kadhaa na tini.+ 24 Wakapaita mahali hapo Bonde la Eshkoli*+ kwa sababu ya kishada ambacho Waisraeli walikata kutoka huko.
25 Baada ya kuipeleleza nchi kwa siku 40,+ wanaume hao walirudi. 26 Walirudi kwa Musa, Haruni, na Waisraeli wote katika nyika ya Parani, huko Kadeshi.+ Wakawaletea habari Waisraeli wote na kuwaonyesha matunda ya nchi hiyo. 27 Hivi ndivyo walivyomwambia Musa: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, na kwa kweli inatiririka maziwa na asali,+ na haya ndiyo matunda yake.+
-