-
Hesabu 14:39-45Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
39 Musa alipowaambia Waisraeli wote maneno hayo, watu walianza kuomboleza kwa uchungu mwingi. 40 Hata waliamka asubuhi na mapema na kujaribu kupanda juu mlimani, wakisema: “Tuko tayari kupanda mpaka mahali ambapo Yehova alituambia, kwa maana tumetenda dhambi.”+ 41 Lakini Musa akawaambia: “Kwa nini mnakiuka agizo la Yehova? Hamtafanikiwa. 42 Msipande kwenda huko, kwa sababu Yehova hayuko pamoja nanyi; mtashindwa na maadui wenu.+ 43 Kwa maana Waamaleki na Wakanaani watakabiliana nanyi huko,+ nao watawaangamiza kwa upanga. Kwa sababu mliacha kumfuata Yehova, Yehova hatakuwa pamoja nanyi.”+
44 Hata hivyo, kwa kimbelembele wakapanda kuelekea mlimani,+ lakini sanduku la agano la Yehova lilibaki katikati ya kambi, na Musa pia alibaki.+ 45 Ndipo Waamaleki na Wakanaani walioishi kwenye mlima huo wakashuka na kuanza kuwashambulia, wakawatawanya mpaka Horma.+
-