Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 12:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Msimfanyie hivyo Yehova Mungu wenu, kwa sababu mataifa hayo yanaifanyia miungu yao kila jambo linalochukiza ambalo Yehova anachukia, hata kuwateketeza motoni wana na mabinti wao kwa ajili ya miungu yao.+

  • 2 Wafalme 16:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Katika mwaka wa 17 wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi+ mwana wa Mfalme Yothamu wa Yuda akawa mfalme.

  • 2 Wafalme 16:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Badala yake, alitembea katika njia ya wafalme wa Israeli,+ na hata alimteketeza* motoni mwana wake mwenyewe,+ akifuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli.

  • 2 Mambo ya Nyakati 28:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Ahazi+ alikuwa na umri wa miaka 20 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 16 huko Yerusalemu. Hakutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova kama alivyotenda Daudi babu yake.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 28:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Isitoshe, alifukiza moshi wa dhabihu katika Bonde la Mwana wa Hinomu* na kuwateketeza wanawe motoni,+ akifuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli.

  • Zaburi 106:35-37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Lakini walichangamana na mataifa hayo+

      Na kuzikubali* njia zao.+

      36 Waliendelea kuabudu sanamu zao,+

      Nazo zikawa mtego kwao.+

      37 Waliwatoa dhabihu wana wao

      Na mabinti wao kwa roho waovu.+

  • Yeremia 32:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Isitoshe, walijenga mahali pa juu pa Baali katika Bonde la Mwana wa Hinomu,*+ ili kuwateketeza* motoni wana wao na mabinti wao kwa ajili ya Moleki,+ jambo ambalo sikuwaamuru,+ na ambalo halijawahi kamwe kuingia moyoni mwangu,* kufanya jambo kama hilo linalochukiza, na kusababisha watu wa Yuda watende dhambi.’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki