-
Waamuzi 11:17, 18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Kisha Waisraeli wakatuma wajumbe kwa mfalme wa Edomu,+ wakisema, “Tafadhali turuhusu tupitie katika nchi yako,” lakini mfalme wa Edomu akakataa. Kisha wakatuma wajumbe kwa mfalme wa Moabu,+ naye pia akakataa. Basi Waisraeli wakaendelea kukaa Kadeshi.+ 18 Walipopitia nyikani, waliizunguka nchi ya Edomu+ na nchi ya Moabu. Wakapitia upande wa mashariki wa nchi ya Moabu+ na kupiga kambi katika eneo la Arnoni; hawakufika kwenye mpaka wa Moabu kwa sababu Mto Arnoni ulikuwa mpaka wa Moabu.+
-