Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 34:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Muwe waangalifu msifanye agano na wakaaji wa nchi, kwa maana wanapofanya ukahaba na miungu yao na kuitolea dhabihu,+ mmoja wao atawaalika nanyi mtakula dhabihu yake.+

  • Kumbukumbu la Torati 7:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Kwa maana watawapotosha wana wenu waache kumfuata Mungu na kuanza kuabudu miungu mingine;+ kisha hasira ya Yehova itawaka dhidi yenu, naye atawaangamiza upesi.+

  • Yoshua 23:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Lakini mkimwacha na kushikamana na watu wa mataifa haya yaliyobaki+ na kuoana nao+ na kushirikiana nao, 13 mjue kwa hakika kwamba Yehova Mungu wenu hataendelea kuyafukuza* mataifa haya kwa ajili yenu.+ Yatakuwa mtego wa kuwanasa, nayo yatakuwa mjeledi wa kuwachapa mbavuni+ na miiba machoni mwenu mpaka mtakapoangamia kutoka katika nchi hii nzuri ambayo Yehova Mungu wenu amewapa.

  • Isaya 2:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Kwa maana umewaacha watu wako, nyumba ya Yakobo,+

      Kwa sababu wamejaa vitu vya kutoka Mashariki;

      Wanafanya uchawi+ kama Wafilisti,

      Nao wana watoto wengi wa wageni.

  • 1 Wakorintho 5:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Kujisifu kwenu hakufai. Je, hamjui kwamba chachu* kidogo huchachisha donge lote?+

  • 1 Wakorintho 15:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Msipotoshwe. Kushirikiana na watu wabaya huharibu tabia nzuri.*+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki