14 Ndipo wanaume hao wakamwambia: “Tutakufa badala yenu!* Ikiwa hamtatoa habari kuhusu mambo yaliyotuleta, tutawatendea kwa upendo mshikamanifu na kwa uaminifu Yehova atakapotupatia nchi hii.”
17 Jiji na vitu vyote vilivyomo vinapaswa kuharibiwa;+ vyote ni vya Yehova. Ila msimwangamize Rahabu+ yule kahaba na wote walio pamoja naye nyumbani mwake, kwa sababu aliwaficha wajumbe tuliowatuma.+
22 Yoshua akawaambia wale wanaume wawili waliokuwa wameipeleleza nchi: “Nendeni katika nyumba ya yule mwanamke kahaba, mkamtoe nje pamoja na watu wake wote, kama mlivyomwapia.”+