Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 13:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Basi Abramu akaendelea kuishi katika mahema. Baadaye akaja na kuishi kati ya miti mikubwa ya Mamre,+ ambayo iko Hebroni,+ na huko akamjengea Yehova madhabahu.+

  • Mwanzo 23:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Baada ya hayo Abrahamu akamzika Sara mke wake katika pango la shamba la Makpela mbele ya Mamre, yaani, Hebroni, katika nchi ya Kanaani.

  • Hesabu 13:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Walipopanda na kuingia Negebu, walifika Hebroni,+ ambako Ahimani, Sheshai, na Talmai,+ wazao wa Anaki+ waliishi. Sasa, Jiji la Hebroni lilijengwa miaka saba kabla ya jiji la Soani lililoko Misri.

  • Yoshua 10:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Basi Adoni-sedeki mfalme wa Yerusalemu akatuma ujumbe huu kwa Hohamu mfalme wa Hebroni,+ Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na kwa Debiri mfalme wa Egloni:+ 4 “Njooni mnisaidie kuwashambulia wakaaji wa Gibeoni, kwa sababu wamefanya amani na Yoshua na Waisraeli.”+

  • Yoshua 15:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Naye Yoshua akampa Kalebu+ mwana wa Yefune sehemu ya nchi kati ya wazao wa Yuda kama Yehova alivyomwagiza Yoshua, yaani, eneo la Kiriath-arba (Arba alikuwa baba ya Waanaki), yaani, Hebroni.+

  • Yoshua 21:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Nao wakawapa wana wa kuhani Haruni jiji la makimbilio kwa ajili ya muuaji,+ yaani, jiji la Hebroni,+ na malisho yake, pia Libna+ na malisho yake,

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki