6Basi Yehova akamwambia Musa: “Sasa utaona mambo nitakayomtendea Farao.+ Mkono wenye nguvu utamlazimisha awaruhusu watu wangu waende zao, na mkono wenye nguvu utamlazimisha awafukuze kutoka katika nchi yake.”+
11Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Nitamletea Farao na Misri pigo moja zaidi. Baada ya pigo hilo atawaruhusu mwondoke hapa.+ Atakapowaruhusu mwondoke, atawafukuza kabisa kutoka hapa.+