Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 8:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 kumbukeni kwamba Yehova Mungu wenu ndiye anayewapa nguvu za kupata utajiri,+ ili atimize agano lake ambalo aliwaapia mababu zenu, kama ilivyo leo.+

  • Kumbukumbu la Torati 28:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Yehova atawafungulia ghala lake zuri, mbingu, ili mvua inyeshe juu ya nchi yenu katika majira yake+ na kubariki kila jambo mnalofanya. Mtayakopesha mataifa mengi, lakini ninyi wenyewe hamtahitaji kukopa.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 1:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Kisha Mungu akamwambia Sulemani: “Kwa sababu moyo wako unatamani jambo hilo, nawe hukuomba mali, utajiri, wala heshima wala hukuomba wale wanaokuchukia wafe, wala hukuomba maisha marefu,* lakini umeomba hekima na ujuzi ili uwahukumu watu wangu ambao nimekuweka uwe mfalme wao,+ 12 nitakupa hekima na ujuzi; lakini nitakupa pia mali na utajiri na heshima, kuliko mfalme yeyote kabla yako na mfalme yeyote baada yako.”+

  • Ayubu 42:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kwa hiyo, Yehova alibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ya kwanza,+ na Ayubu akawa na kondoo 14,000, ngamia 6,000, ng’ombe 2,000,* na punda jike 1,000.+

  • Methali 10:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Baraka ya Yehova ndiyo inayomtajirisha mtu,+

      Naye haichanganyi na maumivu.*

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki