-
2 Samweli 5:23, 24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Daudi akamwomba Yehova ushauri, lakini Akasema: “Usipande moja kwa moja. Badala yake, zunguka nyuma yao, uwashambulie mbele ya vichaka vya mibaka. 24 Na utakaposikia sauti ya watu wakipiga mwendo juu ya vichaka vya mibaka, tenda bila kusita, kwa sababu mimi Yehova nitakuwa nimetangulia mbele yako kuliua jeshi la Wafilisti.”
-
-
2 Wafalme 6:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Mtumishi* wa mtu wa Mungu wa kweli alipoamka asubuhi na mapema na kutoka nje, aliona jeshi lenye farasi na magari ya vita yakiwa yamezunguka jiji. Mara moja mtumishi huyo akamwambia: “Ole wetu, bwana wangu! Tutafanya nini?” 16 Lakini Elisha akamwambia: “Usiogope!+ Kwa maana wale walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.”+
-