18Baada tu ya Daudi kumaliza kuzungumza na Sauli, Yonathani+ na Daudi wakashikamana na kuwa marafiki wa karibu sana,* na Yonathani akaanza kumpenda kama alivyojipenda mwenyewe.*+
2 Kwa kuwa Yonathani mwana wa Sauli alimpenda sana Daudi,+ alimwambia hivi Daudi: “Sauli baba yangu anakusudia kukuua. Tafadhali jihadhari itakapofika asubuhi, nenda mahali pa siri na ujifiche huko.