-
1 Mambo ya Nyakati 10:8-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Siku iliyofuata, Wafilisti walipokuja kuwavua waliouawa vitu walivyokuwa navyo, walimkuta Sauli na wanawe wakiwa wameanguka kwenye Mlima Gilboa.+ 9 Basi wakamvua mavazi yake, wakamkata kichwa na kuchukua silaha zake, nao wakatuma ujumbe kotekote katika nchi ya Wafilisti ili habari hizo zienezwe kwa sanamu+ zao na watu. 10 Kisha wakaweka silaha zake katika nyumba ya* mungu wao na kulitundika fuvu lake kwenye nyumba ya Dagoni.+
11 Wakaaji wote wa Yabeshi+ kule Gileadi waliposikia mambo yote ambayo Wafilisti walikuwa wamemtendea Sauli,+ 12 mashujaa wote wakaondoka na kubeba maiti ya Sauli na maiti za wanawe. Wakawaleta Yabeshi na kuzika mifupa yao chini ya mti mkubwa kule Yabeshi,+ nao wakafunga kwa siku saba.
-