Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 7:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Muda mrefu ulipita, jumla ya miaka 20, tangu Sanduku hilo lilipoletwa Kiriath-yearimu, na nyumba yote ya Israeli kuanza kumtafuta* Yehova.+

  • 1 Wafalme 8:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Wakati huo Sulemani aliwakusanya+ wazee wa Israeli—viongozi wote wa makabila, wakuu wa koo* za Israeli.+ Wakaja kwa Mfalme Sulemani huko Yerusalemu ili kuliondoa sanduku la agano la Yehova katika Jiji la Daudi,+ yaani, Sayuni.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 13:1-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Daudi alishauriana na wakuu wa maelfu na wa mamia na kila kiongozi.+ 2 Kisha Daudi akaliambia kutaniko lote la Waisraeli: “Mkiona ni vema na ikiwa ni jambo linalokubalika kwa Yehova Mungu wetu, acheni tutume ujumbe kwa ndugu zetu waliobaki katika maeneo yote ya Israeli na pia kwa makuhani na Walawi katika majiji yao+ yenye malisho waje kuungana nasi. 3 Na acheni tulirudishe Sanduku+ la Mungu wetu.” Kwa maana hawakuwa wamelitunza katika siku za Sauli.+ 4 Kutaniko lote likakubali kufanya hivyo, kwa maana watu wote waliliona kuwa jambo jema. 5 Basi Daudi akawakusanya Waisraeli wote, kuanzia mto wa Misri* mpaka Lebo-Hamathi,*+ ili walete Sanduku la Mungu wa kweli kutoka Kiriath-yearimu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki