-
1 Mambo ya Nyakati 17:16-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Ndipo Mfalme Daudi akaingia na kuketi mbele za Yehova na kusema: “Mimi ni nani, Ee Yehova Mungu? Na nyumba yangu ni nini hivi kwamba umenileta mpaka hapa nilipofika?+ 17 Na kana kwamba hilo halitoshi, Ee Mungu, unasema pia kwamba nyumba yangu mimi mtumishi wako itadumu kwa muda mrefu,+ nawe umeniona kuwa mtu anayepaswa kukwezwa zaidi,* Ee Yehova Mungu. 18 Mimi mtumishi wako Daudi nitakwambia nini zaidi kuhusu heshima uliyonipa na wewe unanijua vizuri sana mimi mtumishi wako?+ 19 Ee Yehova, kwa ajili yangu mimi mtumishi wako na kupatana na moyo wako* umetenda mambo haya yote makuu kwa kufunua ukuu wako.+ 20 Ee Yehova, hakuna aliye kama wewe,+ na hakuna Mungu ila wewe;+ mambo yote tuliyosikia kwa masikio yetu yanathibitisha jambo hilo. 21 Na kuna taifa gani lingine duniani lililo kama watu wako Waisraeli?+ Wewe Mungu wa kweli ulienda na kuwakomboa wakiwa watu wako.+ Ulijijengea jina kwa matendo yako makuu na yenye kuogopesha,+ ukayafukuza mataifa kutoka mbele ya watu wako+ uliowakomboa kutoka Misri. 22 Uliwafanya watu wako Waisraeli wawe watu wako milele;+ na wewe, Ee Yehova, ukawa Mungu wao.+
-