-
Kumbukumbu la Torati 23:3-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 “Hakuna Mwamoni au Mmoabu anayepaswa kuja katika kutaniko la Yehova.+ Hata kufikia kizazi cha kumi, hakuna mzao wao yeyote anayepaswa kuja katika kutaniko la Yehova, 4 kwa sababu hawakuwasaidia kwa kuwapa chakula na maji mlipokuwa njiani kutoka Misri,+ na kwa sababu walimkodi Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori kule Mesopotamia ili awalaani ninyi.+ 5 Lakini Yehova Mungu wenu alikataa kumsikiliza Balaamu.+ Badala yake, Yehova Mungu wenu alibadili laana hiyo ikawa baraka kwenu,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu aliwapenda.+ 6 Hampaswi kamwe kuhangaikia hali yao wala kuwasaidia kupata ufanisi siku zenu zote.+
-