-
2 Samweli 14:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Sasa Yoabu mwana wa Seruya+ akatambua kwamba moyo wa mfalme ulitamani kumwona Absalomu.+ 2 Kwa hiyo Yoabu akatuma watu huko Tekoa+ wamlete mwanamke mwerevu, akamwambia hivi: “Tafadhali, jifanye kana kwamba unaomboleza, nawe uvae nguo za kuomboleza, na usijipake mafuta.+ Jifanye kama mwanamke ambaye amekuwa akiomboleza kwa siku nyingi kwa sababu ya kufiwa. 3 Kisha uende kwa mfalme na kumwambia hivi.” Basi Yoabu akamwambia mambo ya kusema.*
-