Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 18:7-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kisha dunia ikaanza kutetemeka na kutikisika;+

      Misingi ya milima ikasukasuka

      Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+

       8 Moshi ulipanda kutoka katika mianzi ya pua yake,

      Na moto unaoteketeza kabisa ukatoka kinywani mwake;+

      Makaa ya mawe yanayowaka moto mkali yakatoka kwake.

       9 Alizifanya mbingu zijikunje alipokuwa akishuka,+

      Na giza zito lilikuwa chini ya miguu yake.+

      10 Alipanda juu ya kerubi, akaja akiruka.+

      Akashuka chini kwa ghafla juu ya mabawa ya kiumbe wa roho.*+

      11 Kisha akajifunika giza,+

      Pande zote kama banda,

      Maji yenye giza na mawingu mazito.+

      12 Kutoka katika mwangaza ulio mbele zake

      Mvua ya mawe na makaa ya mawe yanayowaka moto yakapasua mawingu.

  • Zaburi 77:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Sauti ya mngurumo+ wako ilikuwa kama magurudumu ya gari la vita;

      Mimweko ya radi iliangaza dunia inayokaliwa;*+

      Dunia ilitikisika na kutetemeka.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki