Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 22:8-16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Dunia ikaanza kutetemeka na kutikisika huku na huku;+

      Misingi ya mbingu ikasukasuka+

      Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+

       9 Moshi ulipanda kutoka katika mianzi ya pua yake,

      Na moto unaoteketeza kabisa ukatoka kinywani mwake;+

      Makaa ya mawe yanayowaka moto mkali yakatoka kwake.

      10 Alizifanya mbingu zijikunje alipokuwa akishuka,+

      Na giza zito lilikuwa chini ya miguu yake.+

      11 Alipanda juu ya kerubi,+ akaja akiruka.

      Alionekana juu ya mabawa ya kiumbe wa roho.*+

      12 Kisha akaweka giza kumzunguka kama kibanda,+

      Katika maji yenye giza na mawingu mazito.

      13 Kutoka katika mwangaza ulio mbele zake makaa ya mawe yenye moto mkali yaliwaka.

      14 Kisha Yehova akaanza kunguruma kutoka mbinguni;+

      Aliye Juu Zaidi aliifanya sauti yake isikike.+

      15 Alipiga mishale yake+ akawatawanya;

      Radi, akawavuruga.+

      16 Sakafu ya bahari ikaonekana;+

      Misingi ya nchi ikafunuliwa kwa kemeo la Yehova,

      Kwa mlipuko wa pumzi kutoka katika mianzi ya pua yake.+

  • Zaburi 77:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Sauti ya mngurumo+ wako ilikuwa kama magurudumu ya gari la vita;

      Mimweko ya radi iliangaza dunia inayokaliwa;*+

      Dunia ilitikisika na kutetemeka.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki