Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Mambo ya Nyakati 21:18-23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Ndipo malaika wa Yehova akamwambia Gadi+ amwambie Daudi apande na kumjengea Yehova madhabahu kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Ornani Myebusi.+ 19 Basi Daudi akapanda kulingana na neno la Gadi, alilosema katika jina la Yehova. 20 Wakati huo, Ornani akageuka na kumwona huyo malaika, na wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha. Wakati huo Ornani alikuwa akipura ngano. 21 Daudi alipopanda na kufika kwake, Ornani alitazama na kumwona Daudi, mara moja akatoka kwenye uwanja wa kupuria na kumwinamia Daudi kifudifudi. 22 Daudi akamwambia Ornani: “Niuzie* uwanja wa kupuria ili nimjengee Yehova madhabahu kwenye uwanja huo. Niuzie kwa bei kamili, ili ugonjwa hatari ambao umewakumba watu ukomeshwe.”+ 23 Lakini Ornani akamwambia Daudi: “Uchukue uwe wako, bwana wangu mfalme fanya lolote unaloona ni jema.* Tazama, ninatoa ng’ombe kwa ajili ya dhabihu za kuteketezwa na kifaa cha kupuria+ utakachotumia kama kuni na ngano ya toleo la nafaka. Ninatoa vitu hivi vyote.”

  • 2 Mambo ya Nyakati 3:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kisha Sulemani akaanza kujenga nyumba ya Yehova+ huko Yerusalemu juu ya Mlima Moria,+ mahali ambapo Yehova alikuwa amemtokea Daudi baba yake,+ mahali ambapo Daudi alikuwa ametayarisha kwenye uwanja wa kupuria wa Ornani Myebusi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki