-
Nehemia 13:25-27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Ndipo nikawakemea na kuwalaani, nikawapiga baadhi ya wanaume hao,+ nikazing’oa nywele zao na kuwaapisha hivi kwa Mungu: “Msikubali mabinti wenu waolewe na wana wao, na msikubali mabinti wao waolewe na wana wenu au ninyi wenyewe.+ 26 Je, Mfalme Sulemani wa Israeli hakutenda dhambi kwa sababu yao? Hakukuwa na mfalme kama yeye miongoni mwa mataifa mengi;+ naye alipendwa na Mungu wake,+ hivi kwamba Mungu akamweka kuwa mfalme wa nchi yote ya Israeli. Lakini wake wa kigeni walimfanya hata yeye atende dhambi.+ 27 Je, si jambo linaloshangaza kwenu kutenda uovu huu mkubwa kwa kutokuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni?”+
-