-
2 Mambo ya Nyakati 1:3-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Kisha Sulemani na Waisraeli wote wakaenda mahali pa juu kule Gibeoni,+ kwa maana hema la mkutano la Mungu wa kweli lilikuwa huko, hema ambalo Musa mtumishi wa Yehova alitengeneza nyikani. 4 Hata hivyo, Daudi alikuwa amelipandisha Sanduku la Mungu wa kweli kutoka Kiriath-yearimu+ na kulileta mahali ambapo Daudi alikuwa ametayarisha kwa ajili yake; alikuwa amepiga hema kwa ajili ya Sanduku hilo huko Yerusalemu.+ 5 Na ile madhabahu ya shaba+ ambayo Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru alikuwa ametengeneza ilikuwa imewekwa mbele ya hema la ibada la Yehova; na Sulemani na Waisraeli wote walikuwa wakisali mbele yake.* 6 Kisha Sulemani akamtolea Yehova dhabihu mahali hapo, alitoa dhabihu 1,000 za kuteketezwa kwenye madhabahu ya shaba+ ya hema la mkutano.
-