-
2 Mambo ya Nyakati 6:28-31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
28 “Njaa kali ikitokea nchini,+ au ugonjwa hatari,+ upepo unaochoma, kuvu,+ makundi ya nzige, au parare* wanaokula sana+ au maadui wao wakiwazingira katika jiji lolote nchini*+ au pigo au ugonjwa wa aina yoyote ukitokea,+ 29 sala yoyote,+ ombi lolote la kutaka kibali+ ambalo huenda likatolewa na mtu yeyote au na watu wako wote Waisraeli (kwa sababu kila mmoja anajua mateso yake mwenyewe na maumivu yake mwenyewe)+ wakinyoosha mikono yao kuelekea nyumba hii,+ 30 basi usikie kutoka mbinguni, makao yako,+ nawe usamehe;+ na umthawabishe kila mmoja kulingana na njia zake zote, kwa sababu unajua moyo wake (ni wewe peke yako unayejua vizuri moyo wa mwanadamu),+ 31 ili wakuogope kwa kutembea katika njia zako sikuzote watakazoishi katika nchi uliyowapa mababu zetu.
-