-
2 Mambo ya Nyakati 18:12-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Basi mjumbe aliyeenda kumwita Mikaya akamwambia: “Tazama! Manabii wote kwa pamoja wanasema mema kumhusu mfalme. Tafadhali, acha neno lako liwe kama maneno yao,+ useme mema.”+ 13 Lakini Mikaya akasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, jambo lolote ambalo Mungu wangu atasema ndilo nitakalosema.”+ 14 Kisha akaingia kwa mfalme, naye mfalme akamuuliza: “Mikaya, je, twende kupigana vita dhidi ya Ramothi-gileadi, au nisiende?” Mara moja akajibu: “Panda uende nawe utafanikiwa; watatiwa mikononi mwako.” 15 Ndipo mfalme akamuuliza: “Nitakuapisha mara ngapi kwamba hupaswi kuniambia jambo lingine lolote isipokuwa ukweli katika jina la Yehova?” 16 Basi Mikaya akasema: “Ninawaona Waisraeli wote wakiwa wametawanyika milimani, kama kondoo wasio na mchungaji.+ Yehova akasema: ‘Hawa hawana bwana. Acha kila mmoja wao arudi kwa amani nyumbani kwake.’”
-