Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 2:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kisha akachukua vazi rasmi la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwake, akayapiga maji na kuuliza: “Yuko wapi Yehova, Mungu wa Eliya?” Alipoyapiga maji, yaligawanyika kushoto na kulia, Elisha akavuka ng’ambo.+

  • 2 Wafalme 2:20, 21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Akawaambia: “Nileteeni bakuli dogo jipya, mweke chumvi ndani yake.” Basi wakamletea. 21 Kisha akatoka na kwenda kwenye chemchemi ya maji hayo, akatupa chumvi ndani yake+ na kusema: “Yehova anasema hivi: ‘Nimeyaponya maji haya. Hayatasababisha tena kifo wala utasa.’”*

  • 2 Wafalme 3:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 kwa maana Yehova anasema hivi: “Hamtaona upepo, wala hamtaona mvua; hata hivyo bonde* hili litajaa maji,+ nanyi mtakunywa maji yake, ninyi, ng’ombe wenu, na wanyama wenu wengine.”’

  • 2 Wafalme 4:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Kisha uingie nyumbani mwako pamoja na wanao na kufunga mlango. Jaza vyombo hivyo vyote, na uweke kando vilivyojaa.”

  • 2 Wafalme 4:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwa hiyo mwanamke huyo akaenda kwa yule mtu wa Mungu wa kweli, mtu huyo akamwambia: “Nenda, yauze mafuta hayo ulipe madeni yako, nawe pamoja na wanao mnaweza kuishi kwa kile kinachobaki.”

  • 2 Wafalme 6:5-7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Mmoja wao alipokuwa akikata mti, shoka likaanguka majini, akasema kwa sauti: “Ole wangu, bwana wangu, liliazimwa!” 6 Mtu wa Mungu wa kweli akauliza: “Limeanguka wapi?” Basi akamwonyesha mahali hapo. Ndipo Elisha akakata kipande cha mti na kukitupa hapo, akalifanya shoka lielee. 7 Akasema: “Lichukue.” Akaunyoosha mkono wake na kulichukua.

  • 2 Wafalme 7:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Sasa Elisha akasema: “Sikiliza neno la Yehova. Yehova anasema hivi: ‘Kesho karibu wakati kama huu sea moja* ya unga laini itakuwa na thamani ya shekeli moja, na sea mbili za shayiri zitakuwa na thamani ya shekeli moja* katika lango la* Samaria.’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki