-
2 Mambo ya Nyakati 21:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Katika siku zake, Waedomu waliasi nchi ya Yuda+ na kujichagulia mfalme wao wenyewe.+ 9 Basi Yehoramu na makamanda wake wakavuka na magari yake yote ya vita, naye akaondoka usiku na kuwashinda Waedomu waliokuwa wamemzingira yeye na makamanda wake wa magari ya vita. 10 Lakini tangu siku hiyo Waedomu wameendelea kuiasi nchi ya Yuda. Watu wa Libna+ pia walimwasi Yehoramu wakati huo, kwa sababu alikuwa amemwacha Yehova Mungu wa mababu zake.+
-